Buriani Hayati Richard Said Nyaulawa
RAIS Jakaya Kikwete pamoja na mkewe Mama Salma jana aliongoza mamia ya waombolezaji wakiwamo viongozi wa serikali, wabunge na wananchi kuaga mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Vijijini, Richard Nyaulawa (57) aliyefariki dunia Jumapili nyumbani kwake, Kawe Beach, Dar es Salaam. Mwili wa marehemu Nyaulawa uliagwa kwa Ibada ya Misa iliyoongozwa na Paroko wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Martha, Mikocheni, Padri Paul Haule na kisha heshima hizo za mwisho. Nyaulawa anatarajiwa kuzikwa leo kijijini kwao InyalaMbeya vijijini.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi -AMEN
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi -AMEN
0 comments:
Post a Comment