will smith atua Bongo kimya kimya
mwigizaji mchekeshaji na mwanamuziki will smith na mai waifu wake jada pinckett smith wametua dar kinyemela na mchana huu wameelekea kula vekesheni huko zenji. michuzijr.blogspot.com alikuwepo hoteli ya kempinski kilimanjaro na kuwabamba wakielekea kupanda gari lililowapeleka uwanja wa ndege wa eapoti ya julius nyerere. habari zinasema will smith alimuulizia lady jd na baada ya kumkosa kwa kuwa alikuwa studio akirekodi albamu yake mpya, akaacha maagizo kuwa bibie huyo afanye juu chini waonane akirejea toka zenj
Picha zote hizi toka Michuzi Blog
0 comments:
Post a Comment